Posts

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO NOVEMBA 14,2025

Image
 

MKAKATI WA MAWASILIANO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA: DIRA YA MAFANIKIO YA TAIFA – MHANDISI KABUNDUGURU

Image
Aeleza Mkakati huo ni mwongozo wa kitaifa kwa wadau wote Atoa wito kwa Maafisa dawati kuwa chachu ya mabadiliko ya Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia Taasisi zilizo chini ya Wizara zaeleza zinavyotekeleza mkakati wa Taifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia Na Mwandishi wetu,MWANZA IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni dira muhimu ya kufanikisha malengo ya Taifa ya kuhakikisha wananchi  wanatumia nishati salama, rafiki wa mazingira na yenye gharama nafuu hadi kufikia mwaka 2034. Hayo yameelezwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia Wizara ya Nishati, Mhandisi Banezeth Kabunduguru wakati wa kuhitimisha mafunzo kwa Maafisa Dawati na Waratibu wa Nishati Safi ya Kupikia wa Kanda ya Ziwa, yaliyofanyika jijini Mwanza tarehe 14 Novemba, 2025. Kabunduguru amefafanua kuwa, mkakati huo umekusudiwa kuwa mwongozo wa kitaifa utakaowaongoza wadau wote katika kutoa elimu sahihi, iitayofika kwa urahisi kwa wananchi wa  makundi mba...

ELIMU YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUOKOA MAISHA ZAIDI YA ELFU 33 KILA MWAKA NCHINI

Image
Wizara ya Nishati yasema elimu kwa maafisa dawati italeta mapinduzi ya kiafya na kimazingira Mikoa ya Kanda ya Kati na Kaskazini wanufaika na elimu Maafisa Dawati kutumia elimu hiyo kutekeleza azma ya Serikali Na Mwandishi wetu SIGINDA ELIMU ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia inayotolewa na Wizara ya Nishati kwa maafisa dawati na waratibu wa nishati safi ya kupikia katika halmashauri na mikoa yote nchini, inatarajiwa kuokoa vifo vya watu zaidi ya 33,000 kila mwaka vinavyotokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia. Hayo yameelezwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia Wizara ya Nishati, Mhandisi Banezeth Kabunduguru wakati akiwasilisha mada katika mafunzo ya maafisa hao yaliyofanyika mkoani Singida tarehe 12 Novemba 2025. Kabunduguru amefafanua kuwa, kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 takribani watu 33,024 hufariki kila mwaka nchini Tanzania kutokana na athari za matumizi ya nishati isiyosafi ya kupikia. “Zaidi ya watu milioni 3...

MBUNGE MAVUNDE AANZISHA UJENZI WA ZAHANATI MTAA WA MASEYA-HOMBOLO MAKULU

Image
Wananchi wanampongeza kwa kutimiza ahadi yake Aapa ujenzi kwa wakati Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa visima vya umwagiliaji na Umeme Na Mwandishi wetu MBUNGE wa Jimbo la Mtumba Mh. Anthony Mavunde leo ameshiriki na mamia ya wananchi wa Mtaa wa Maseya-Kata ya Hombolo Makulu ujenzi wa Zahanati katika mtaa huo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa Uchaguzi Mkuu 2025. “Nawashukuru wananchi wa Maseya kwa kumchagua Rais Samia,mimi na Diwani wa kata yetu kwa kura nyingi sana kwenye uchaguzi mkuu uliomalizika. Kazi yetu sasa ni kufanya kazi na kutatua changamoto za wananchi, tunawapongeza kwa kuitikia wito wa ujenzi wa zahanati yetu ambayo ofisi yetu iko kusogeza karibu huduma ya Afya kwa wananchi wetu. Nitakabidhi kutuma 2000 na saruji mifuko 100 ili kulifikisha jengo letu mpaka hatua ya upauaji,ni imani yangu serikali yetu sikivu itatuunga mkono ukamilishaji wa zahanati hii”Alisema Mavunde. Akitoa salamu za wananchi,Mwenyekiti wa Mtaa wa Maseya Alexander Fwalu amemshukuru Rais...

MAKUSANYO YA MADINI SIMIYU YAVUKA MALENGO, YAFIKIA ZAIDI YA ASILIMIA 103

Image
Na Mwandishi wetu, SIMIYU AFISA Madini Mkazi wa Mkoa wa Simiyu, Mayigi Makolobela, amesema mkoa huo umeendelea kufanya vizuri wakati wa kuzingatia yatokanayo na Sekta ya Madini, ambapo makusanyo ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 yamevuka malengo kwa kufikiria zaidi ya asilimia 103 ya lengo lililowekwa kwa kipindi husika. Akizugumza mkoani Simiyu, Makolobela amesema kwa mwaka wa fedha uliopita, ofisi yake ilipewa lengo la kukusanya Shilingi bilioni 4, lakini walifanikiwa kukusanya zaidi ya Shilingi bilioni 4.5. “Kwa mwaka huu wa fedha tumewekewa lengo la kukusanya Shilingi bilioni 4.76, na hadi kufikiria robo ya kwanza tayari kukusanya zaidi ya Shilingi bilioni 1.23, sawa na asilimia 103 ya lengo la robo mwaka,” amesema Makolobela. Ameongeza kuwa tangu kuanzia Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, makusanyo ya madini kupitia wachimbaji wadogo mkoani humo yamefikia zaidi ya Shilingi bilioni 17, hatua inayodhihirisha ukuaji na uimara wa sekta hiyo katika ...

DKT.MHANDO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA MTAKUWWA II DODOMA

Image
  Na Mwandishi wetu KAMISHNA  wa Ustawi wa Jamii Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Nandera .E. Mhando ameongoza kikao cha Kamati tendaji ya Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto Awamu ya Pili (MTAKUWWA II), kilichofanyika tarehe 11 Novemba, 2025 Jijini Dodoma. kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe kutoka Wizara, Taasisi za Serikali Taasisi za Kifedha na Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa ambacho kimejadili na kupitia taarifa ya Utekelezaji wa MTAKUWWA II ya kwa mwaka 2024/2025.

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

Image
Na Mwandishi Wetu, Riyadh Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 26 wa Baraza Kuu la Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism) kilichoanza leo Novemba 9, 2025, jijini Riyadh, Saudi Arabia, nimeihakikishia dunia kuwa hali ya utalii na amani imara nchini Tanzania kufuatia machafuko yaliyotokea wakati baada ya uchaguzi katika baadhi ya maeneo. Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo wakati akichangia Taarifa ya Utekelezaji wa Mwaka wa Taasisi hiyo ambapo pia Tanzania ilinufaika na programu mbalimbali ikiwemo kuandaa Mkutano wa Dunia Kanda ya Afrika wa Utalii wa Vyakula vya Arusha April mwaka huu na kufadhiliwa baadhi ya programu za utunzaji wa mazingira katika maeneo ya Safu za Milima ya Usambara. “Mheshimiwa Mwenyekiti wa Baraza hili baada ya kumpongeza Katibu Mkuu na Sekretarieti ya UN Tourism kwa utekelezaji ambao Tanzania pia imenufaika, naomba kutumia fursa hii kutoa taarifa kuwa Tanzania ni salama ya kadhia iliyojitokeza wak...