e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI
Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa wananchi Na Mwandishi wetu WATAALAMU kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wameisifu TANESCO kwa mafanikio makubwa ya matumizi ya teknolojia katika utoaji huduma kwa wateja, hatua iliyochangia kuongeza ufanisi na kuwahudumia wananchi kwa haraka zaidi. Wakizungumza wakati wa ziara katika Kituo cha miito ya simu (Call Center) Julai 23, 2026, wataalamu hao walieleza kuvutiwa na mifumo ya kidigitali inayotumiwa na TANESCO kupokea, kufuatilia na kutatua changamoto za wateja, ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii kufikisha taarifa na kupokea mrejesho kwa wakati. Kwa upande wake, Meneja wa Kituo cha Huduma kwa Wateja TANESCO, Shamu Lameck, alisema ziara hiyo ni fursa ya kubadilishana uzoefu na kuonesha hatua ambazo Shirika limefikia katika kutumia teknolojia kuboresha huduma kwa wateja. Aliongeza kuwa kutambuliwa kwa TANESCO kama kituo cha kujifunzia na taasisi mbalimbali kunathibitisha mafanikio...