Posts

NLD YAPONGEZA MSAJILI, DOYO ATAKA UWAJIBIKAJI WA KISASA KWA VYAMA VYOTE BILA UBAGUZI

Image
    Na Mwandishi wetu, TANGA CHAMA cha National League for Democracy (NLD) kimesema hatua ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuvitaka vyama vya CCM na CHADEMA kutoa maelezo kuhusu kauli za baadhi ya viongozi wao ni ishara ya usimamizi wa haki na usawa kwa vyama vyote vya siasa nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga leo, Katibu Mkuu wa NLD, Doyo Hassan Doyo, alisema uamuzi huo unaonyesha kuwa sheria na taratibu za kisiasa zinaweza kutekelezwa kwa usawa bila kuangalia ukubwa au nguvu ya chama husika. Doyo alieleza kuwa hatua ya Msajili kuviandikia barua vyama hivyo viwili imeondoa hisia za upendeleo ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara katika utekelezaji wa sheria zinazohusu vyama vya siasa. Aliongeza kuwa utekelezaji wa sheria kwa usawa unasaidia kuimarisha imani ya wananchi kwa taasisi zinazosimamia mfumo wa kisiasa pamoja na kudumisha misingi ya haki, uwajibikaji na utawala wa sheria. Pamoja na hayo, NLD limewataka viongozi wa kisiasa pamoja na wana...

TMA NA BRAC MAENDELEO TANZANIA WAJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA USAMBAZAJI NA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA

Image
  Na Mwandishi wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  na BRAC Maendeleo Tanzania walifanya kikao Makao Makuu ya TMA jijini Dodoma, wakijadili mikakati ya kuimarisha usambazaji na matumizi ya taarifa za hali ya hewa nchini.  Kikao hicho kiliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a, kwa kuwakaribisha wajumbe wa BRAC Maendeleo Tanzania na kueleza kuwa TMA inathamini ushirikiano na wadau katika kuboresha huduma za hali ya hewa.  Alisema mkutano huo unatoa fursa ya taasisi hizo mbili kuelewana na kuchunguza maeneo ya ushirikiano katika huduma za hali ya hewa, tahadhari za mapema na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Pia alieleza kuwa TMA ipo katika mageuzi ya kidigitali yanayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa njia za kisasa. Dkt. Chang’a Alieleza dhamira ya TMA kuendelea kuboresha huduma za hali y...

TMA YATOA ELIMU YA HALI YA HEWA KWA WAVUVI KUPITIA MRADI WA ECOFISH

Image
Na Mwandishi wetu MRADI wa ECOFISH unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Denmark kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Shirika la Denmark la Maendeleo ya Kimataifa (DANIDA), unaendelea kuboresha shughuli za uvuvi kwa jamii ya Pwani na kuimarisha huduma za tahadhari za mapema za hali ya hewa nchini. Katika utekelezaji wa mradi huo, wataalamu kutoka TMA walikutana na wavuvi pamoja na wakulima wa Mwani kwa lengo la kujionea hali halisi ya shughuli zao za kiuchumi na changamoto zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa  wanazokabiliana nazo, sambamba na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa katika shughuli za uvuvi na kilimo cha Mwani.  Ziara hiyo iliambatana na semina maalum iliyowakutanisha wavuvi na wakulima wa Mwani ikiwa ni sehemu ya juhudi za mradi huo katika kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika kufanya maamuzi sahihi na salama. Akizungumza katika semina hiyo, Mtaalamu...

NONDO KUMPELEKA BABA LEVO MAHAKAMANI

Image
Na Mwandishi wetu MWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya ACT Wazalendo, Abdul Omary Nondo ametangaza kumfungulia kesi ya madai ya kashfa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Clayton Revocatus Chipando maarufu "Baba Levo" akimtuhumu kusambaza taarifa za uongo zinazodai kuwa alijiteka mwenyewe katika matukio mawili tofauti ya utekaji yaliyowahi kumkuta. Nondo ameyabainisha hayo Jijini Dar es salaam mapema leo Mei 23, 2026 wakati akizugumza na waandishi wa habari ambapo mesema Baba Levo amekuwa akitoa kauli hizo kupitia vyombo vya habari, mahojiano pamoja na mitandao ya kijamii, jambo ambalo amesema limemchafua, kumdhalilisha na kuvunja heshima yake mbele ya jamii. Amesema Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa pamoja na Mahakama Kuu tayari zilishatoa maamuzi yaliyomuondoa hatiani katika kesi iliyokuwa ikimkabili mwaka 2018 kuhusu madai ya kujiteka, huku rufaa ya mwisho iliyowasilishwa Mahakama ya Rufani ikiondolewa mwaka 2022 baada ya upande wa mashtaka kueleza kutokuwa na nia ya kuendelea nayo....

MKURUGENZI WA RASILIMALI WATU TANESCO AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO MAAFISA HUDUMA KWA WATEJA KUBORESHA UTENDAJI

Image
   Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao Awapongeza kwa utendaji bora wenye kujenga taswira chanya ya Serikali na Shirika kwa wananchi Na Mwandishi wetu  MKURUGENZI wa Rasilimali Watu na Utawala TANESCO,  Beatrice Kimoleta, amewahakikishia Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja ushirikiano katika kufanikisha upatikanaji wa nyenzo muhimu zitakazowawezesha kuhudumia wateja kwa ufanisi na ubora wa hali ya juu. Ametoa kauli hiyo Mei 22, 2026 alipokuwa akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa maafisa hao uliofanyika kwa siku tano kuanzia Mei 18, 2026  jijini Dodoma, mkutano ambao hufanyika kila mwaka kwa lengo la kufanya tathmini ya kuboresha utendaji kazi wa kurugenzi ili kufanikisha malengo yaliyowekwa. “Kwa uongozi wa Shirika, kipaumbele chetu ni kuhakikisha watumishi wanaohudumia wateja moja kwa moja wanakuwa katika mazingira mazuri ya kazi ili waweze kutoa huduma kwa ufanisi. Tunawahakikishia kuwapatia nyenzo muhimu ili muendelee kutoa huduma bora kwa wateja,” ame...

RIO FERDINAND:"SIPO HAPA KWA AJILI YA SIASA, NIPO KUWAHAMASISHA VIJANA

Image
  NYOTA wa zamani wa Klabu ya Manchester United na timu ya Taifa ya Uingereza, Rio Ferdinand, amekanusha kuhusika na siasa wakati wa ziara yake nchini Tanzania, akisisitiza kuwa lengo lake kubwa ni kuhamasisha  Vijana wenye vipaji na mapenzi kwenye soka. Rio amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari, Mei 22, 2026  Jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Mwenyeji wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Paul Makonda. "Napenda kusisitiza kwamba mimi si mwanasiasa sipo hapa kuzungumzia siasa, sijawahi kufanya hivyo hata katika nchi yangu mwenyewe, na siwezi kufanya hivyo mahali pengine popote" alisisitiza Rio. Ziara ya Rio imelenga kuimarisha maendeleo ya soka la vijana wa kitanzania kupitia taasisi yake iliyoko nchini Uingereza huku akiweka wazi dhamira yake ya kujenga akademia ya michezo hapa nchini. Kwa upande wake Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Paul Makonda amesema, ndoto yake ilikuwa ni kumleta Mchezaji Rio Ferdinand...

MD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE

Image
Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme  Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa Mradi huo Na Mwandishi Wetu, Korogwe, Tanga MKURUGENZI Mtendaji wa TANESCO  Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022.  Twange ameyasema hayo leo Mei 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati. “Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange. Amesema mr...