Posts

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

Image
Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa wananchi Na Mwandishi wetu WATAALAMU kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wameisifu TANESCO kwa mafanikio makubwa ya matumizi ya teknolojia katika utoaji huduma kwa wateja, hatua iliyochangia kuongeza ufanisi na kuwahudumia wananchi kwa haraka zaidi. Wakizungumza wakati wa ziara katika Kituo cha miito ya simu (Call Center) Julai 23, 2026, wataalamu hao walieleza kuvutiwa na mifumo ya kidigitali inayotumiwa na TANESCO kupokea, kufuatilia na kutatua changamoto za wateja, ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii kufikisha taarifa na kupokea mrejesho kwa wakati. Kwa upande wake, Meneja wa Kituo cha Huduma kwa Wateja TANESCO, Shamu Lameck, alisema ziara hiyo ni fursa ya kubadilishana uzoefu na kuonesha hatua ambazo Shirika limefikia katika kutumia teknolojia kuboresha huduma kwa wateja. Aliongeza kuwa kutambuliwa kwa TANESCO kama kituo cha kujifunzia na taasisi mbalimbali kunathibitisha mafanikio...

NEWALA KUNUFAIKA NA UMEME WA UHAKIKA

Image
Ni baada ya kukamilika kwa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 Masasi - Mtwara  Mradi umeimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Wilaya ya Newala na wananchi. MD Twange asema thamani ya mradi takribani shilingi bilioni 4.65 Newala, Mtwara | Julai 21, 2026 WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amezindua rasmi mradi wa njia ya kusafirisha kilovoti 33, akieleza mradi huo katika sehemu za Serikali za kuendelea kufikia kufikia uhakika kwa wananchi kuweka mazingira wezeshi kwa shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Newala. Mawasiliano wakati wa njia hiyo,  Ndejembi amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ya umeme ili kuhakikisha huduma ya nishati inawafikia wananchi wengine zaidi na kuwa chachu ya maendeleo. "Njia hii ya umeme ni msingi wa kukuza uchumi, kuongeza mchango, kuboresha kuboresha ubora kwa Wilaya ya Newala," amesema Mhe. Ndejemb...

SADC KUJA TANZANIA KUJIFUNZA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
  Na Mwandishi wetu  TANZANIA imeendelea kuthibitisha nafasi yake ya uongozi katika ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia barani Afrika, huku nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) zikieleza nia ya kuja nchini kujifunza mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa agenda hiyo. Pia, SADC imeipongeza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kumtambua Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uongozi wake mahiri na mchango mkubwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, katika Kanda na Afrika kwa ujumla. Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Pamoja wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji wa nchi wanachama wa SADC uliofanyika kwa njia ya mtandao Julai 17, 2026.: Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza kwa mafanikio Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034, ambapo matumizi ya nishati safi ya kupiki...

RAIS DKT. MWINYI AJIONEA MAFANIKIO YA TANESCO MAONESHO YA SABASABA

Image
  Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar  Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi. Akitoa maelezo...

TBA YANG'ARA KWA TUZO YA BANDA BORA SABASABA

Image
  Na Mwandishi wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umetunukiwa tuzo ya mshindi wa nafasi ya pili katika kipengele cha banda bora upande wa Sekta ya Miliki na Majengo Na Ardhi (Real Estate) wakati wa sherehe za ufungaji wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba). Kilele cha maonesho hayo kilifikia Julai 13, 2026 katika Viwanja vya Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam zikiongozwa na Rais wa Zanzibar, na Dkt Hussein Ali Mwinyi kufunga na kutoa tuzo kwa washindi. Aidha tuzo ya TBA imepokelewa kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa TBA, Daud Kondoro, na Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Amina Lumuli. Akizugumza Lumuli amesema ushindi huo unatokana na ubunifu mkubwa uliooneshwa katika maandalizi ya banda la taasisi hiyo pamoja na namna lilivyofanikiwa kuwasilisha fursa mbalimbali za uwekezaji kwa wananchi na wadau wa maendeleo. "TBA imeweka mkazo katika kuonesha fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), pamoja na kuelimisha ...

MD TWANGE -UKOPESHAJI MAJIKO UMEME UMEFANIKIWA KWA ASILIMIA 90

Image
Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Lazaro Twange amesema amemweleza Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi hatua zinazochukuliwa na shirika hilo katika kutekeleza mkakati wa nishati safi ya kupikia, ikiwemo utekelezaji wa mpango wa kukopesha majiko ya umeme kwa wananchi kupitia mfumo wa Bill Financing. Twange amesema hayo wakati akizungumzia mambo muhimu aliyomueleza Rais Wa Zanzibar, Dkt Hussein Ali Mwinyi alipotembeleza banda hilo lililopo katika maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa maarufu kama Sabasaba. Amesema mpango huo unawawezesha wateja wapya pamoja na waliopo kupata majiko ya umeme kwa mkopo na kulipa taratibu kupitia ununuzi wa umeme. "Kwa sasa tuna mpango unaoitwa Bill Financing ambao unaendelea. Wateja wetu wapya na wale ambao tayari wanatumia umeme wanaweza kukopeshwa majiko na wakawa wanalipa mkopo wao kadri wanavyonunua umeme," amesema. Amesema mpango huo umepata mwitikio mkubwa na kufikia mafanikio ya zaidi ya asilimia 90, hali iliyo...

WANANCHI WAENDELEA KUNUFAIKA NA OFA ZA TTCL SABASABA 2026

Image
  Na Mwandishi wetu MAAFISA  wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wanaendelea kuwahudumia wananchi wanaotembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), kwa kuwapatia elimu kuhusu huduma na suluhisho mbalimbali za mawasiliano na teknolojia za kidijitali zinazotolewa na TTCL. Katika banda hilo, wananchi wanapata fursa ya kujionea huduma za intaneti ya kasi ya juu, suluhisho za kidijitali kwa matumizi ya nyumbani na biashara, pamoja na kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali zinazotolewa na TTCL. Sambamba na hilo, TTCL inaendelea kuwapatia wateja ofa maalum za Sabasaba, zikiwemo vifaa vya mawasiliano vinavyopatikana kwa bei zenye punguzo kubwa, pamoja na huduma mbalimbali zinazolenga kurahisisha maisha na shughuli za kila siku katika mazingira ya kidijitali. Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Banda Janeth Maeda amesema ushiriki wa Shirika katika Sabasaba 2026 unalenga kuwasogezea wananchi...