MCHUMI FLORIAN KARUGABA AJITOSA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KIVULE.
Na Mwandishi wetu
MCHUMI Frolian Karugaba amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge Jimbo la Kivule kupitia Chama cha Mapinduzi CCM.
Karugaba ambaye pia ni Mwezeshaji wa wafugaji wa kuku ,amechukua fomu mapema leo Juni 29,2025 na kukabidhiwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Ilala, Sylvester Yeredi.
Karugaba amesema amejitosa kugombea ubunge jimbo la Kivule kutatua changamoto mbalimbali za jimbo hilo kwani dhamira ya Serikali kuondoa kero hivyo atakaposhinda ubunge atatatua kero za wananchi ambapo alisema ana uwezo mkubwa akishinda ubunge atasimamia uwezeshaji wananchi kiuchumi waweze kunufaika.


Comments
Post a Comment