MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA
Na Mwandishi wetu
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres yaliyofanyika kando ya Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari unaofanyika Jijini Nice nchini Ufaransa Juni 10, 2025.
Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha zaidi ushirikiano baina ya Tanzania na Umoja wa Mataifa kupitia Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Umoja wa Mataifa.



Comments
Post a Comment