MCHUNGAJI HANANJA: TUILINDE AMAMI ILIYOPO NCHINI
Na Mwandishi wetu,
MCHUNGAJI Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Richard Hananja ametoa wito kwa viongozi wa dini na watanzania kuhakikisha wanalinda na kutunza amani iliyopo nchini.
Mchugaji Hananja ametoa wito huo Jijini Dar es salaam mapema leo Juni 9, 2025 wakati akizugumza na waandishi wa habari.
Amesema amani ikitoweka nchi inaweza ikasambaratika na kusababisha sitofahamu.
"Kukosoa sio tatizo Bali tatizo ni namna ya kukosoa kwamba kinapaswa kuwa kwa adabu na sio kutukana na kuzomea"amesema
Aidha aliishauri Serikali kuwa makanisa yote yanayokiuka taratibu kupingwa pini..huku alisisitiza yafate taratibu zilizowekwa.



Comments
Post a Comment