MWANASHERIA JOHN PETER AJITOSA UBUNGE JIMBO LA UKONGA
Na Mwandishi wetu
MWANASHERIA John Peter amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Ubunge Jimbo la Ukonga kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Peter amechukua fomu hiyo mapema leo Julai 1,2025 na kukabidhiwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Ilala, Sylvester Yeredi.
Peter amesema endapo atapata ridhaa ya kuteuliwa na Chama atahakikisha anatatua chagamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo hilo.


Comments
Post a Comment