TASAC YATOA ELIMU YA USALAMA WA USAFIRI MAJINI SABASABA
Na Mwandishi wetu
SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limesema litaendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya usalama wa usafiri majini jinsi unavyochagia katika uchumi wa Nchi.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa bodi ya wakurungezi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC ) Naodha Mussa Mandia alipotembelea Banda la TASAC lililopo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea sabasaba wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii juu ya usafiri wa majini unavyochagia katika uchumi wa Nchi .
Amesema TASAC ina jukumu la kudhibiti na kusimamia usalama,ulinzi wa usafirishaji majini ambao ni kiungo kikuu katika kukuza uchumi.
"TASAC inayo majukumu mawili moja la Udhibiti na lingine kuamasisha watu kushiriki katika ulinzi na usalama na usafiri na usafirishaji kwa njia ya maji"amesema
Amesema majukum mengine ya TASAC ni pamoja na kuhakikisha meli zote zinazotia nanga kwa ajili ya kuleta bidhaa mbalimbali nchini zinakuwa salama pamoja na kulinda mazingira ya bahari.
Akizungumzia kuhusu maonesho ya Sabasaba amesema TASAC inashiriki katika maonesho hayo kutoa elimu kwa wananchi inavyohakikisha usalama na ulinzi wa bandari zote nchini.
Katika hatua nyingine Kapteni Mandia amesema
hali ya usalama wa bahari ni shwari na TASAC imekuwa ikishirikiana na vyombo usalama katika maeneo hayo kupitia vyombo vya ulinzi na usalama




Comments
Post a Comment