BANDA LA TAA LAFANA NANENANE,KAIMU MKURUGENZI WA TMA ATEMBELEA.
Na Mwandishi wetu
KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Ladislaus Chang'a ametembela Banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania( TAA) katika Maonyesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni Dodoma. Dkt, Chang'a ameipongeza TAA kwa kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa katika Viwanja vya ndege hapa nchini.
Maonyesho ya Kilimo ya Nanenane yanaongozwa na kauli mbiu " Chagua viongozi bora kwa Maendeleo ya kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025".


Comments
Post a Comment