KAMATI KUU CCM YAMPITISHA MASABURI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KIVULE.



Na Mwandishi Wetu

CHAMA Cha MapinduziCCM (CCM) kimempitisha mwanachama wa mwaka ambaye pia aliwahi kuwa Naibu katika Meya ya Halmashauri ya Manispaa ya ilala Ojambi Didas Masaburi kuwa Mgombea ubunge wa Jimbo la Kivule jijini Dar es Salaam katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba huu

Masaburi ambaye aliongoza mchakato wa kura za maoni ya Chama hicho ametangazwa kuwa ndani Jimboni baada ya Kamati Kuu ya CCM kukaa kikao Dodoma na kuchuja majina ya ubunge wake ambao watapeperusha bendera katika Uchaguzi huo.

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) CPA Amoss Makalla ametangaza majina ya ubunge katika majimbo yote ambapo jimbo la Kivule Mgombea ubunge aliyepitishwa na Chama hicho ni Ojambi Masaburi .

Baada ya kupitishwa kwa jina lake Masaburi atachukua fomu ya kugombea ubunge na kisha kuirejesha katika Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na hatimae kusubiria kampeni kwa ajili ya kuomba kura kwa wananchi katika Jimbo la Kivule.

Kwa kukumbusha tu Jimbo la Kivule ni Jimbo jipya ambalo limepatikana baada ya Tume Huru ya Uchaguzi kuligawa Jimbo la Ukonga na kupatikana majimbo mawili  ambayo  Ukonga na Kivule na Jimbo hilo la Kivule Mgombea wake ni Masaburi.

Comments

Popular posts from this blog

WANAFUNZI WALIOMALIZA KIDIA SEKONDARI WACHANGIA UJENZI WA KANISA SH MILLION 20

VETA YAJIPANGA KUSHIRIKINA NA TOYOTA TANZANIA KUIMARISHA MAFUNZO YA UFUNDI MAGARI

UJENZI WA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MTO MALAGARASI , WAPIGA HATUA MPYA