MGOMBEA URAIS NRA AKABIDHIWA FOMU NA INEC
Na Mwandishi wetu
MWENYEKITI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, leo Agosti 9, 2025, amemkabidhi fomu ya uteuzi Mgombea wa Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA), Hassan Kisabya Almas.
Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi za Tume zilizopo Njedengwa, Jijini Dodoma, ambapo Almas aliambatana na Mgombea Mwenza wa nafasi ya Makamu wa Rais kupitia chama hicho, Hamis Ali Hassan.



Comments
Post a Comment