MKUTANO MKUU MAALUM WA UVCCM KUPIGA KURA ZA MAONI KUCHAGUA WABUNGE VIJANA LEO
Na Mwandishi wetu
UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) unawakaribisha Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa kura za Maoni wa kuwachagua Wabunge Vijana unaofanyika Leo tarehe 1 Agosti, 2025 katika Ukumbi wa Jiji, Jijini Dodoma.
Mkutano huo utahudhuriwa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa UVCCM Taifa ambao ni Wanawake tu kutoka katika Mikoa na Wilaya za Tanzania Bara na Visiwani ili kupata Wabunge 10 wa Viti Maalumu; Wabunge 6 Kwa Bara na Wabunge 4 Kwa upande wa Tanzania Zanzibar pamoja na Wajumbe 2 wa Baraza la Wawakilishi.
Ni Mkutano uliobeba ndoto za Vijana wa Kitanzania kuhakikisha wanapata Wabunge mahiri Kwa ajili ya Maendeleo ya Vijana Tanzania.
Vijana Tunasema OKTOBA TUNATIKI
#KaziNaUtuTunasongaMbele #TunazimaZoteTunawashaKijani


Comments
Post a Comment