MTENDAJI MKUU WMA ATEMBELEA MAONESHO YA NANENANE DODOMA

 



Na Mwandishi wetu

OFISA Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) Alban Kihulla, leo Agosti 8, 2025 ametembelea Maonesho ya NaneNane kitaifa, uwanja wa Nzuguni jijini Dodoma.

Akiwa katika Banda la WMA, Afisa Mtendaji Mkuu amewapongeza watumishi wa Wakala kwa kazi nzuri ya kuelimisha umma ambao wamekuwa wakiifanya tangu kuanza kwa Maonesho hayo.

Amewataka kuendelea kutoa elimu kwa jamii hata baada ya Maonesho ili wananchi waelewe ni kwa namna gani kupitia WMA inawalinda Serikali kwa vipimo vinavyotumika katika sekta mbalimbali ni sahihi na vinatumika kwa matumizi. 




"Tuendelee kutumia majukwaa mbalimbali kutoa elimu ya vipimo kwa wananchi ili waelewe haki yao ya kupata huduma kwa vipimo sahihi lakini pia na wajibu wao wa kushughulikia wanatumia vipimo sahihi katika sekta mbalimbali.

Kihulla ametembelea mabanda mengine likiwemo banda la Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Taasisi zake ili kujionea huduma zinazotolewa.

Comments

Popular posts from this blog

WANAFUNZI WALIOMALIZA KIDIA SEKONDARI WACHANGIA UJENZI WA KANISA SH MILLION 20

VETA YAJIPANGA KUSHIRIKINA NA TOYOTA TANZANIA KUIMARISHA MAFUNZO YA UFUNDI MAGARI

UJENZI WA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MTO MALAGARASI , WAPIGA HATUA MPYA