UZALISHAJI UMEME KWA KUTUMIA NISHATI JADIDIFU UMEFIKIA ASILIMIA 67- KAMISHNA LUOGA



Amshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya Nishati Jadidifu

Mafunzo ya mafunzo ya teknolojia ya Nishati ya Jua kwa wataalamu


Na Mwandishi wetu

TANZANIA imeendelea kuongeza vyanzo vya nishati kwa kutumia nishati jadidifu hadi asilimia 67, ikijumuisha matumizi ya nishati ya maji na Jua.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga wakati akifunga mafunzo ya wataalam kutoka taasisi mbalimbali zilizohusu usanifu, kuweka na ufungaji wa kanuni za Nishati ya Jua pamoja na matumizi yake.




"Tanzania imepiga hatua kubwa katika matumizi ya jadidifu ikiwa ni pamoja na Ni Safi ya hasa baada ya kuweka saini Mpango Mahsusi wa Taifa wa Nishati mwezi wa Januari huu, moja ya miradi mikubwa tunayoitekeleza sasa katika sikukuu jadidifu ni mradi wa umeme jua wa Kishapu mkoani Shinyanga ambao wamefikia asilimia 75 na unatarajiwa kutarajiwa katika awamu ya 50 ya awamu ya kwanza." Amesema Luoga

Akifunga mafunzo hayo  Mhandisi Luoga amesema mafunzo kuhusu nishati ya Jua yamefanyika nchini kwa sababu Tanzania imepiga hatua kubwa katika matumizi ya nishati na jadidifu.

Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya Nishati Jadidifu nchini.

Amesema washiriki kutoka katika taasisi mbalimbali wameshiriki mafunzo ya Nishati ya Jua yanayojulikana kama SOLTRAIN + ambayo yameandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kitengo cha Kituo Mahiri cha Matumizi Bora ya Nishati na Nishati Jadidifu (SACREE) ambayo kipo chini ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi zilizo Kusini mwa Afrika ( SADC).



Awali, mafunzo hayo yalifunguliwa na Mhandisi Felchesmi Mramba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ambapo aliwataka washiriki ujuzi na maarifa waliyopata katika kujiajiri na pia kutoa ujuzi kwa wengine.


Comments

Popular posts from this blog

WANAFUNZI WALIOMALIZA KIDIA SEKONDARI WACHANGIA UJENZI WA KANISA SH MILLION 20

VETA YAJIPANGA KUSHIRIKINA NA TOYOTA TANZANIA KUIMARISHA MAFUNZO YA UFUNDI MAGARI

UJENZI WA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MTO MALAGARASI , WAPIGA HATUA MPYA