DKT. MWINYI ANENA NA VIONGOZI WA DINI PEMBA
Na Mwandishi wetu
SERIKALI ya chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar inasimamia Amani, umoja, Haki na Maridhiano, na Ndio njia pekee yakuwafanya Wananchi wake waweze kuwa wamoja, na kuahidi kuendelea kuhakikisha Amani na Utulivu inatawala kipindi chote cha Uchaguzi Mkuu utafanyika October 29.
Akizungumza na Viongozi wa Dini katika Ukumbi Uliopo Skuli ya UTAANI wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, ikiwa ni Muendelezo wa Kampeni zake za kuomba Ridhaa ya kuiongoza tena Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi Ameahidi kuyafanyia Kazi Masuala yote yaliyowasilishwa na Viongozi wa Dini zote katika Mkutano huo na kuwasihi Kuilinda Amani iliyopo Kwani ni Wajibu wa kila mmoja


Comments
Post a Comment