MASHINDANO YA DUNIA YA KUHIFADHI QURAAN KUFANYIKA KWA MKAPA APRIL 5
Na Mwandishi wetu
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemmed Suleiman Abdulla anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika nufusu fainali ya Mashindano ya Dunia ya Kuhifadhi Quraan Tukufu kwa washiriki wa ndani.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kuhifadhisha Quraan Tanzaniam, Sheikh Othuman Kapolo, amesema nusu fainali hiyo itafanyika Aprili 2 mwaka huu katika Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege, Unguja, Zanzibar.
Sheikh Kapolo amesema nusu fainali hiyo ni kuele fainali ya mashindano hayo itakayofanyika Aprili 5mwaka huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
"Tayali washiriki wa fainali hiyo kutoka mataifa mbalimbali duniani wameanza kuwasili nchini.Hadi kufikia Ijumaa wiki hii tunatarajia tutakuwa tumepokea washiriki wote 26 kutoka mataifa mbalimbali duniani yaliyothibitishwa kushiriki,"ameeleza Shekh Kapolo.
Amesema jumla ya zawadi zote kwa washindi ni sh. milioni 125 ambapo pia kutakuwa na zawadi kwa wananchi watakaofika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Aprili 25 kushuhudia fainali hiyo, ambazo ni pamoja na simu za mkononi, pikipiki, pikipiki za mizigo 'Guta' na tiketi za umra.
Awali, akizungumza kwa niaba ya Mwakilishi wa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dk. Aboubakar Zuberi, Sheikh Hassan Chizenga, amesema mashindano hayo ya Dunia ya Kuhifadhi Quraan yamekuwa alama ya kuitambulisha Tanzania kitaifa na kimataifa hivyo kuwataka wananchi wote bila kujali itikadi zao za kidini kushuhudia.

Comments
Post a Comment