NDEJEMBI AONGOZA KIKAO CHA KUWEKA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA BAJETI NA HOJA ZA WABUNGE.

 

lol



Na Mwandishi wetu

WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, pamoja na Naibu Waziri wa Nishati,  Salome Makamba wamekutana na Viongozi wa Wizara pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara kwa kuweka makumbusho ya utekelezaji wa hoja Makala yaliyotolewa na Wabunge, pamoja na kujipanga kwa utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Waziri Ndejembi na Naibu Waziri Salome wamekutana na Viongozi hao katika kikao cha kwanza cha kimkakati mara baada ya Bajeti kupitishwa, kilichowashirikisha Makatibu Wakuu, Makamishna, Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Wenyeviti wa Bodi za Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Taasisi na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Nishati.

Katika kikao hicho, Waziri Ndejembi amewataka viongozi wa kila idara na vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake, kila mmoja kujipanga kimkakati katika utekelezaji wa mambo yote yaliyoahidiwa kupitia Bajeti, pamoja na kutafuta majawabu na utekelezaji wa maoni na kumbukumbu ya Waheshimiwa Wabunge yaliyotolewa wakati wa Baraza.





Aidha, Ndejembi ametoa wito kwa Watumishi wote kutekeleza majukumu kwa kutimiza ahadi na maono ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwahudumia wananchi na kuwafikishia huduma bora na maendeleo kupitia sekta ya nishati.






Comments

Popular posts from this blog

WANAFUNZI WALIOMALIZA KIDIA SEKONDARI WACHANGIA UJENZI WA KANISA SH MILLION 20

VETA YAJIPANGA KUSHIRIKINA NA TOYOTA TANZANIA KUIMARISHA MAFUNZO YA UFUNDI MAGARI

UJENZI WA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MTO MALAGARASI , WAPIGA HATUA MPYA